Friday, November 30, 2012

Tembo/Elephants

Tembo/Elephants

Uwindaji haramu wa Faru/Tembo


Uwindaji haramu dhidi ya Faru na Tembo umeelezwa kuongezeka kwa kiasi kikubwa Barani Afrika. Hayo yamesemwa na Dk Joseph Okori ambaye ni Kiongozi wa Mpango wa kunusuru Faru kwa upande wa Afrika chini ya WWF.

Dk Okori alisema kuwa maelfu ya tembo na Farau takribani 588 wameuawa kwa kipindi cha mwaka huu wa 2012. “Faru wanaweza kupotea kabisa kwa kipindi cha miaka 10 kama hatutachukua hatua za kukomesha ujangili huo,” alisema Dk Okori.

Alisema kuwa nchini Afrika ya Kusini Faru wanauawa kila siku kutokana na uhitaji mkubwa wa pembe zao. Dk Okori alieleza kuwa Asia ndiyo soko kubwa la pembe hizo za Faru  na hasa nchini Vietnam. Aliongeza kuwa kiasi kikubwa cha pembe za tembo zinasafirishwa kwenda nchini Thailand na China.
(source: http://wwf.panda.org/?206876/Only-10-years-left-to-save-rhinos)



Maoni ya Katiba Mpya

Sophia Mateo Mkazi wa Bunju: Katiba ipige marufuku ubakaji wa watoto. Sophia Mateo a resident of Bunju: The Constitution should ban child rape

Sophia Seme mkazi wa Bunju: Muungano wetu umekuwa mfano bora Barani Afrika, nataka uendelee kama ulivyo: Our union with Zanzibar has been a good example in Africa, I suggest it to remain as it is.

Ally Chambuso mkazi wa Bunju: Wageni wasipewe maeneo ambayo wananchi wanakaa au kuyatumia: The Constitution should prohibit investors to be given the areas used by the citizen

Mkazi wa Bunju akitoa maoni yake ya Katiba

Mikidadi Likunguni

Joseph Matonya

Wakazi wa Kata ya Bunju wakifuatilia na kushiriki katika utoaji wa maoni ya Katiba Mpya. The residents of Bunju Ward are participating in the meeting of  Constitutional Review Commission

Saturday, November 24, 2012

Judge Joseph Warioba

Jaji Mstaafu Joseph Warioba akiongea na wakazi wa Upanga Mashariki waliofika kutoa maoni yao ya Katiba Mpya. The retired Judge Joseph Warioba cum the Chairman of the Tanzania Constitutional Review Commission is addressing the residents of Upanga East who gathered at the Office of Local Government Officer for the purpose of airing their opinions on the formation of the New Tanzania Constitution.

Friday, November 23, 2012

Constitutional Review


Hamad: We need alternative imprisonment 

Mbaraka Hamad (49) a businessman from Kisutu Ward in Dar es Salaam, today  he told the Commission of the Constitutional Review that the new Constitution should stop the tendency of the Tanzanian courts to imprison people with minor cases because it is expensive to keep them. He said the cost of keeping one prisoner is about Sh 350,000 per month.

Hamad suggested that the new Constitution should allow the sentenced people to serve their punishments by reporting to the local government officers. He said this is a better way to correct them and to reduce congestion in prisons.

“We need the new Constitution to come up with alternative sentences to people with such minor cases as stealing mangoes or chicken. There is no need to send them into prison. The government spends so much money to keep them. I suggest they should be given alternative imprison and they have to report every day to the local government officers until they finish their punishment,” said Hamad.

Wednesday, November 21, 2012

Vinyago vya chuma/Iron carvings

Manispaa ya Ilala ikiwasisitiza wakazi wa Jiji la Dar es Salaam kuzingatia usafi ili Jiji liwe la kuvutia zaid. The Ilala Municipality insists on the habit of keeping the City clean to the residents of Dar es Salaam.

Maoni ya Katiba/Constitution

Bw Patia Kibwana akitoa maoni yake mbele ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba katika Kata ya Tabata Kimanga Jijini Dar es Salaam Jana. Mr Patia Kibwana (69) was giving his opinions to the Constitutional Review Commission at Tabata Kimanga in Dar es Salaam yesterday.

Monday, November 19, 2012

CCM WAPONGEZANA


Chama Cha Mapinduzi chajipanga kurejesha imani kwa wananchi

Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Dar es Salaam jana kimefanya mkutano mkubwa katika viwanja vya Mnazi Mmoja Jijini Dar es Salaam kwa nia ya kuipongeza Sekretarieti mpya ya Chama hicho. Mkutano huo uliohudhuriwa na wanachama wake kutoka  Wilaya za Temeke, Ilala na Kinondoni waliofika kwa wingi walivifanya viwanja hivyo vya Mnazi Mmoja kulipuka kwa shangwe ya vigelegele, ngoma na nyimbo mbali mbali.
Waliopongezwa kupitia mkutano huo ni Rais Jakaya Kikwete aliyechaguliwa tena kushika nafasi ya Uenyekiti wa Chama kitaifa na Philip Mangula akiwa Makamu Mwenyekiti Bara. Dk Ali Mohamed Shein Makamu Mwenyekiti Zanzibar. Wengine ni Abdulhaman Kinana alichaguliwa kuwa Katibu Mkuu na Mwigulu Nchemba Naibu Katibu Mkuu Bara, wakati Nape Nnauye alichaguliwa kuendelea na nafasi yake ya Katibu Mwenezi wa Chama. 
Rais Kikwete alisema Sekretarieti Mpya kwa kushirikiana na wana CCM wote nchini wana wajibu wa kurejesha imani ya watanzania kwa Chama hicho. Alisema kuwa huu ni wakati wa kufanya tathmini ya kutosha na kuchukua maamuzi ya kuhakikisha kuwa wananchi wanakiunga mkono CCM kama ilivyokuwa zamani.
“Tunapaswa kufanya tathmini ni kujua nini Chama chetu kimefanya mpaka kimekuwa na sura hiyo iliyokuwa nayo sasa kwa jamii. Tutafute sababu ili kuwafanya wananchi waweze kukiunga mkono tena,” alisema Rais Kikwete.
Pia ameitaka Sekretarieti hiyo kufanya mikutano ya hadhara na mikutano ya ndani kama mkakati wa kujijenga upya. Aliwataka kuzunguka nchi nzima na kuzungumza na wanachama na wananchi ili kurejesha tena imani ya wananchi kwa CCM.
Naye Makamu Mwenyekiti, Philipo Mangula alisema kuwa yeye kama Mwenyekiti wa Kamati ya Maadili ya Chama hicho atahakikisha ndani ya miezi sita wala rushwa na watoa rushwa watashughulikiwa vyema ili kukisafisha Chama. Alisema wote ambao wamepata uongozi kwa njia ya rushwa hawataachwa salama na hatua kali zitachukuliwa dhidi yao.
“Tutashughulikia malalamiko yote ndani ya miezi sita. Wote walioingia madarakani kihalali  hao wataendelea lakini wale waliotumia rushwa hatutasubiri polisi au Takukuru, hao hawataendelea ni lazima tuwatoe nje ya uongozi. Mlima nyanya kurudi kazini basi juje ipo kazi,” alisisitiza Mangula.
Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Chama hicho Abdulahaman Kinana alisema kuwa majukumu waliyonayo ni kuisimamia Serikali. Alisema Chama hakiwezi kutimiza wajibu huo ikiwa kuna rushwa, upendeleo na mizengwe. “Kuna tatizo la mmomonyoko wa maadili ndani ya Chama. Hatuwezi kusimamia uadilifu kama sisi wenyewe siyo waadilifu. Tutasimamia katiba yetu, kanuni na maelekezo  ya vikao vizuri,” alisema Kinana.
Alisisitiza kuwa uongozi ndani ya Chama siyo ajira ila ni kujitolea. Alisema kuwa kukijenga Chama ili kukirudishia heshima kama ilivyokuwa awali.

CCM MEMBERSCCCC

CCM MEMBERS

Friday, November 16, 2012

Msiba wa Mzee Venant Hinju

Watoto na wajukuu wa Marehemu Mzee Venant Urban Hinju wakitoa sala yao za mwisho baada ya mazishi. The children and grandchildren of the late Venant Urban Hinju are giving their last prayer after burial ceremony.

Wajukuu wa marehemu wakiongozwa na Daniel Mwingira  na Baby Hinju wakiweka maua kwenye kaburi la babu yao. The grandchildren of the late Venant Hinju are putting flowers on the tomb of their grandfather (Posted by Daniel Mwingira)

Wednesday, November 14, 2012

Mahubiri/Preachings

Paroko Msaidizi wa Mwananyamala Fr Minde akihubiri wakati wa misa kwenye Jumuiya ya Mtakatifu Martin wa Tur Jana. Assistant Parish Priest of Mwananyamala, Fr Minde preaches during the mass at St. Martin Small Christian Community

Waumini wakiimba kwa furaha/ Chirstian are joyfully singing during the mass

Wanakwaya/Quire

Watoto wakifuatilia mahubiri/Chidren are attentively listening to the preachings of Fr Minde

Tuesday, November 13, 2012

Waumini wakisikiliza mahubiri/ Christians are listening to the preachings of Fr Minde

Waumini/Christians

Taka taka kila mahali/ Filth everywhere

Taka taka zimekuwa kero kwa wakazi wa Tandale kwa Alimaua Jijini Dar es Salaam, zinamwagwa kwenye makazi ya watu na zinaweza kuchukua hata wiki nzima bila kuondolewa na kuzagaa hovyo barabarani. Filth is dumped in residential areas at Tandale Alimaua in Dar es Salaam and it spreads near to the road with bad smell. The Local government does not bother removing it immediately.

Sunday, November 11, 2012

Mkutano wa GNLD/ GNLD Meeting at Ubungo Plaza

Andrew Bugembe kutoka Uganda akiwaeleza wageni waalikwa namna bidhaa za GNLD zinavyoweza kumkinga mtu asipate maradhi mbali mbali kama vile saratani. Andrew Bugembe 1 Diamond Director of GNLD was lecturing the invited guests on how bad eating habits can lead to cancerous disease at Ubungo Plaza in Dar es Salaam.

Waalikwa/Invitees

Wageni waalikwa wakisikiliza na kufuatilia kwa makini maelezo kutoka kwa Andrew Bugembe kuhusu faida za kuwa mwanachama wa GNLD. The invitees are closely following Mr Andrew Bugembe who lectured them on the advantages of becoming a GNLD Member.

Maelezo kwa wageni

Mwanachama wa Kampuni ya GNLD akiwaeleza watu walioalikwa kujiunga na kampuni hiyo namna bidhaa zao zinavyofanya kazi. Tukio hilo lilifanyika jana Ubungo Plaza Dar es Salaam. GNLD Staff is explaining to the invitees the importance of using their products. The event took place yesterday at Ubungo Plaza in Dar es Salaam

Saturday, November 10, 2012

Police wakidhibiti wananchi

Polisi wakiwadhibiti wananchi waliofika katika Hospitali ya Temeke Jijini Dar es Salaam kushuhudia watu waliosemekana kunasana katika tendo la ndoa. Police in Dar es Salaam are in the control of  people who went to witness a man and a woman at Temeke Hospital who are said to be glued superstitiously in adultery.

MV KIGAMBONI

MV Kigamboni ikiwa katika safari zake za kawaida za kusafirisha abira kati ya Posta na Kigamboni Jijini Dar es Salaam. MV Kigamboni  serves people between Posta and Kigamboni in the City of Dar es Salaam, Tanzania. 

Thursday, November 8, 2012

Miraculous Stone

Huu siyo mlima ila ni jiwe. Jiwe hili linaitwa 'MBUJI' na linapatikana katika Kata ya Maguu Wilayani Mbinga. Wenyeji wanasema Jiwe hili lina miujiza mingi. This is not a mountain, it is a stone. It is found at Maguu Ward in Mbinga District in Tanzania. The Indigenous say that the stone is miraculous and it is used as a sacred place for making offerings to their gods.

DATA Center Training in Dar es Salaam

Washiriki wa mafunzo ya mifumo ya kompyuta wakimfuatilia kwa makini Mkufunzi wao. Data Center Trainees are carefully listening to their Lecturer Mehdi Paryavi.The training is being conducted at Kempinsiki Hotel in Dar es Salaam, Tanzania.

IDCA Lecturer

Mkufunzi wa mifumo ya kuhifadhi taarifa kwenye mfumo kompyuta. Mehdi Paryavi -IDCA Lecturer and the President of TechXact Group Corporation

Training continues


Training continues

Washiriki wakichukua notes. Trainees take notes

Monday, November 5, 2012

Wanaume Kazini/ Men at work

Kijiko kikiwa kimetitia kwenye matope wakati kikisafisha mtaro wa maji barabara ya Tandare Uzuri karibu na kituo cha daladala cha Mtogole huku wananchi wakisaidia kukikwamua. Excavator has sunk into mud as it was cleaning the trench along Tandale Uzuri-Sinza road nearby Mtogole  bus stand.

Saturday, November 3, 2012

TBS Essay Participants/Washiriki

Wanafunzi walioshiriki shindano la insha lililotolewa na Shirika la Viwango nchini-TBS kutoka shule za sekondari wakiwa wakiwa kwenye picha ya pamoja na walimu na walezi wao. Students who participated in essay competition which was conducted by Tanzania Bureau of Standards (TBS) are in a get together photo with their teachers and guardians.





Ngoni People dance Lizombe

Wananchi wa Kata ya Mkako Wilayani Mbinga wakicheza ngoma inayoitwa Lizombe wakati Tume ya Mabadiliko ya Katiba ilipofika kuchukua maoni yao hivi karibuni. Ngoma hii inachezwa na Wangoni. The indigenous of Mkako ward in Mbinga district play their Ngoni traditional dance called Lizombe when the Commission of the Constitutional Review went to take their opinions.



Maji Maji Heroes

Mnara wa kumbukumbu ya Mashujaa wa Vita vya MajiMaji uliopo katika Manispaa ya Songea Mkoani Ruvuma. Wananchi na wageni kutoka nje ya nchi hufika hapa kwa ajili ya kujifunza historia ya vita hivyo. The Memorial of Maji Maji War Heroes in Songea Municipal. Maji Maji war against German colonialism in Southern Tanzania happened in 1905-1907.